Lyrics

Diamond Platnumz Ongeza Lyrics


Diamond Platnumz Ongeza Lyrics

Diamond Platnumz Ongeza Lyrics

STREAM/DOWNLOAD MP3 HERE

Mmmmh….
(Ayo Lizer)

Mi kwako sikuingia miguu
Mikono hadi kichwa 
Kiufupi mazima
Nikiamini wa kufa kuzikana

Yaani hoi sio nafuu
Mututi kabisa hata mashaka sina 
Ukiamini 
Utatengwa na Maulana

Mvumilivu hula mbivu 
Nimengoja mpaka zikaoza
Naambulia maumivu 
Ningali sina wa kunipoza

Sijui yangu stahimilivu
Kunyenyekea waniponza
Napambania utulivu
Mwezangu chuki unaikoza

Sikukufuta tu machozi
Ulipolia nililia na wewe
Sasa mbona wanilipa majonzi
Yaani stress mapombe mi nilewe

We ndo wangu Yesu Mkombozi
Sa mbona Petro unaniacha mwenyewe
Nikose usingizi na njozi 
Ndo ufurahi okay sawa

Si unataka nitukanwe
Ongeza ongeza bado
Nidhalilike
Ongeza ongeza bado

Nikose pa kuificha sura
Ongeza ongeza bado
Marafiki wanicheke, waning’onge ada
Ongeza ongeza bado

Mmmh kisichokuua hukukomaza
Ati ikiwa sikani huo msemo nakataa
Maana jua linapoangaza na sina afadhali
Mi kwangu ni mabalaa

Oooh najitahidi kumsinga mwali
Ila somo ananikataa
Oooh penzi letu si la kibatari
Anayamwaga mafuta taa

Kutwa ni vurugu ndani
Purukushani hapakaliki
Roho inaniuma yaani
Kwanini sa tunagombana sweetie

Oooh njema gani 
Niambie labda nitende kipi? (Aah)
Hata pa kucheka hunnie
Ati utani unapanic

Naelewa riziki mafungu saba
Na la kwangu sita
Naelewa sikutoshi labda 
Kukuridhisha

Sikukufuta tu machozi
Ulipolia nililia na wewe
Sasa mbona wanilipa majonzi
Yaani stress mapombe mi nilewe

We ndo wangu Yesu Mkombozi
Sa mbona Petro unaniacha mwenyewe
Nikose usingizi na njozi 
Ndo ufurahi okay sawa

Si unataka nitukanwe
Ongeza ongeza bado
Nidhalilike
Ongeza ongeza bado

Nikose pa kuificha sura
Ongeza ongeza bado
Ndugu jamaa wanicheke, waning’onge ada
Ongeza ongeza bado

Aah nikose pa kuificha sura
Waning’onge ada

(Wasafi)

mp3 button

Subscribe to MX TV

Do you find Morexlusive useful? Click here to give us five stars rating!

Leave a Comment